Genesis 49:8-12


8 “Yuda, ndugu zako watakusifu;
mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako;
wana wa baba yako watakusujudia.

9 Ee Yuda, wewe ni mwana simba;
unarudi toka mawindoni, mwanangu.
Kama simba hunyemelea na kulala chini,
kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?

10 Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda,
wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake,
hadi aje yeye ambaye milki ni yake,
ambaye utii wa mataifa ni wake.

11 Atamfunga punda wake katika mzabibu,
naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi;
atafua mavazi yake katika divai,
majoho yake katika damu ya mizabibu.

12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai,
meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.

Copyright information for SwhKC